IMANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI
Binadamu wote ni sawa, kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake, Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru.
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
Chama cha Mapinduzi (CCM) kilizaliwa tarehe 5 Februari, 1977 kutokana na kuvunjwa kwa vyamavya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP).
HABARI MPYA
- KIKWETE: HATMA YA CCM IPO MIKONONI MWA VIJANA - Tuesday, May 26, 2015
- RATIBA YA UCHAGUZI WA DOLA KWA WANACCM - Tuesday, May 26, 2015
- RATIBA YA MCHAKATO WA URAIS CCM YATAJWA - Monday, May 25, 2015
MADHUMUNI YA CHAMA CHA MAPINDUZI-
Malengo na madhumuni ya chama cha Mapinduzi yatakuwa yafuatayo:-
MWONGOZO WA CCM 1981
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU 2010- 2015
MWELEKEO WA SERA ZA CCM KATIKA MIAKA YA 2010 HADI 2020
SERA ZA MSINGI ZA CHAMA CHA MAPINDUZI
Malengo na madhumuni ya chama cha Mapinduzi yatakuwa yafuatayo:-
MWONGOZO WA CCM 1981
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU 2010- 2015
MWELEKEO WA SERA ZA CCM KATIKA MIAKA YA 2010 HADI 2020
SERA ZA MSINGI ZA CHAMA CHA MAPINDUZI
ZIARA YA KINANA WILAYA YA CHEMBA YAFANA SANA
read more
TUESDAY, NOVEMBER 25, 2014
KINANA ATINGA MASASI, ATAKA CCM IENDELEE KUIBANA SERIKALI JUU YA WAFUJAJI WA FEDHA ZA UMMA
Kadi zilizorudishwa kutoka kwa wananchama wa vyama pinzani ambao kwa hiyari yao leo wamerudi na kujiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana uliofanyika kwenye kijiji cha Chiungutwa wilayani Masasi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi ya aliyekuwa Katibu Mwenezi wa chama cha NLD Taifa Ndugu Frank Rashid Maulano aliyejiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Chiungutwa jimbo la Lulindi wilayani Masasi.
FRIDAY, OCTOBER 31, 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Chama cha Mapinduzi kimepokea kwa furaha matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Msumbiji tarehe 15 Oktoba 2014. Chama Cha Mapinduzi kilikuwa kinafuatilia kwa karibu mchakato wote wa Uchaguzi huo hasa kwa sababu Tanzania na Msumbiji ni nchi zenye uhusiano wa damu.
Kilifuatilia kwa karibu kwa kuwa pia CCM na Chama cha FRELIMO ni vyama ndugu vyenye historia moja na ya pamoja ya Ukombozi Kusini mwa Afrika.
Historia hiyo ndiyo iliyomfanya Rais Mteule wa nchi hiyo Ndugu Filipe NYUSI mara baada ya kuteuliwa kwake na FRELIMO kugombea Urais, nchi ya kwanza kuitembelea kuwa Tanzania.
Ikumbukwe kwamba huyu si mgeni hapa Tanzania. Kama wanaharakati wengine wa ukombozi, Ndugu NYUSI aliishi Tanzania, anaongea vizuri Kiswahili na anaichukulia Tanzania ni nyumbani.
Kwa mnasaba huo, Chama Cha Mapinduzi na Watanzania kwa ujumla tuna kila sababu ya kushangilia ushindi walioupata ndugu zetu wa FRELIMO, kwani ushindi wao ni ushindi wetu.
Tunampongeza sana Rais Mteule Filipe NYUSI kwa kupeperusha vema bendera ya FRELIMO. Matokeo ya Uchaguzi yamedhihirisha imani kubwa waliyonayo wana-Msumbiji kwa FRELIMO na kwa Rais Mteule Filipe NYUSI.
Tuna imani kwamba chini ya uongozi imara wa Mwenyekiti wa CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, na Rais Mteule Filipe NYUSI, uhusiano kati ya vyama vyetu viwili utaimarika na kustawi.
Tunampongeza pia Rais Armando GUEBUZA kwa kuiongoza FRELIMO na Taifa lake vema na kukamilisha uongozi wake kwa mafanikio makubwa. Tunamtakia maisha tulivu ya kiongozi huyo mstaafu.
Anapoanza kipindi hiki cha uongozi wa Taifa lake, sisi wana-CCM tunamtakia Ndugu NYUSI afya njema, busara, maarifa na uongozi uliotukuka.
CCM itasimama pamoja na FRELIMO katika kuendeleza urithi ulioachwa na waasisi wa vyama vyetu Mwalimu Julius NYERERE na Ndugu Samora MACHEL.
Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI
31/10/2014
Ikumbukwe kwamba huyu si mgeni hapa Tanzania. Kama wanaharakati wengine wa ukombozi, Ndugu NYUSI aliishi Tanzania, anaongea vizuri Kiswahili na anaichukulia Tanzania ni nyumbani.
Kwa mnasaba huo, Chama Cha Mapinduzi na Watanzania kwa ujumla tuna kila sababu ya kushangilia ushindi walioupata ndugu zetu wa FRELIMO, kwani ushindi wao ni ushindi wetu.
Tunampongeza sana Rais Mteule Filipe NYUSI kwa kupeperusha vema bendera ya FRELIMO. Matokeo ya Uchaguzi yamedhihirisha imani kubwa waliyonayo wana-Msumbiji kwa FRELIMO na kwa Rais Mteule Filipe NYUSI.
Tuna imani kwamba chini ya uongozi imara wa Mwenyekiti wa CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, na Rais Mteule Filipe NYUSI, uhusiano kati ya vyama vyetu viwili utaimarika na kustawi.
Tunampongeza pia Rais Armando GUEBUZA kwa kuiongoza FRELIMO na Taifa lake vema na kukamilisha uongozi wake kwa mafanikio makubwa. Tunamtakia maisha tulivu ya kiongozi huyo mstaafu.
Anapoanza kipindi hiki cha uongozi wa Taifa lake, sisi wana-CCM tunamtakia Ndugu NYUSI afya njema, busara, maarifa na uongozi uliotukuka.
CCM itasimama pamoja na FRELIMO katika kuendeleza urithi ulioachwa na waasisi wa vyama vyetu Mwalimu Julius NYERERE na Ndugu Samora MACHEL.
Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI
31/10/2014